Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 15 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 183 | 2025-04-30 |
Name
Aleksia Asia Kamguna
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga barabara za Wilaya ya Malinyi kwa kiwango cha lami?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakusudia kujenga kwa tabaka la lami barabara za Makao Makuu ya Wilaya zote hapa nchini ikiwemo Wilaya ya Malinyi. Katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali inaendelea na ujenzi wa Barabara ya Mnadani - Bomani inayoelekea Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi kwa tabaka la lami yenye kilometa 0.85 kwa thamani ya shilingi milioni 759. mpaka sasa ujenzi bado unaendelea na umefikia 30%.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved