Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 15 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 184 | 2025-04-30 |
Name
Neema Gerald Mwandabila
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza kutoa mshahara kwa Madiwani ili waweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa Waheshimiwa Madiwani katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo na huduma za jamii katika mamlaka za Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa, Waheshimiwa Madiwani hulipwa posho za kila mwezi kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Halmashauri na Waraka wa Serikali wa Desemba, 2014 na Waraka wa Aprili, 2015.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia kwamba nafasi ya udiwani ni ya muda maalum wa uongozi na sio ajira ya kudumu inayohusisha utumishi wa moja kwa moja ndani ya mfumo wa Serikali, malipo ya posho yameendelea kuwa njia nzuri ya kutambua mchango wa Waheshimiwa Madiwani, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved