Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Finance and Planning | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 185 | 2025-04-30 |
Name
Joseph Michael Mkundi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Primary Question
MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka Watumishi wa Afya wa kutosha wa Kike - Ukerewe ili kulinda haki ya kijinsia ya Mtoto wa Kike?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya watumishi wa Afya 381. Kati ya hao watumishi 197 ni watumishi wa kike na watumishi 184 ni watumishi wa kiume.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ajira ya Mwaka wa Fedha 2024/2025, Halmashauri ya Ukerewe imepokea watumishi 30 ambapo watumishi 18 ni wa kike na watumishi 12 ni wa kiume. Serikali imekuwa ikizingatia uwiano wa kijinsia wakati wa kuajiri watumishi wa afya na kuwapanga katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved