Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 187 | 2025-04-30 |
Name
Abdallah Jafari Chaurembo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbagala
Primary Question
MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:-
Je, lini tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Kata za Jimbo la Mbagala ikiwemo Chamazi, Mianzini, Kilungule, Charambe, Mbagala, Kiburungwa na Kijichi Mbagala Kuu Maji litaisha?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Jimbo la Mbagala katika maeneo tajwa kunatokana na kuzidiwa kwa Kituo cha Kupoza Umeme cha Mbagala. Ili kutatua changamoto hii, Serikali kupitia TANESCO imefunga transfoma yenye uwezo wa MVA 120 katika kituo hicho na inatarajia kuiwasha hivi karibuni. Aidha, Serikali inatarajia kufunga nyaya zenye uwezo mkubwa katika njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 132 kutoka Kinyerezi hadi Mbagala kupitia Gongolamboto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande mwingine, TANESCO inaendelea na usimamizi wa Mradi wa kuipatia Wilaya ya Mkuranga kituo kikubwa cha kupozea umeme chenye uwezo wa MVA 240 eneo la Dundani na kuacha utegemezi kwenye Kituo cha Mbagala. Kukamilika kwa miradi hii kutasaidia kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Jimbo la Mbagala. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved