Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 15 | Sitting 15 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 190 | 2025-04-30 |
Name
Timotheo Paul Mnzava
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Korogwe Vijijini
Primary Question
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu kwenye Kata za Mkalamo, Magila, Gereza na Kalalani – Korogwe Vijijini?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILINAO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo tarehe 13 Novemba, 2015 Serikali kupitia UCSAF iliingia makubaliano na kampuni ya Honora (Yas) kujenga mnara katika Kata ya Mkalamo. Pia, mnamo tarehe 13 Desemba 2018 UCSAF iliingia makubaliano na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) ili kufikisha mawasiliano katika Kata hiyo ambapo ujenzi wa minara yote miwili ilikamilika kwa kujengwa katika Vijiji vya Magamba na Mpasilasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kutokana na changamoto kubwa katika Kata ya Mkalamo mtoa huduma Honora alijenga minara mingine miwili katika vijiji vya Kwaisewa na Toronto Mbugani na kuifanya Kata hii kuwa na idadi ya minara minne.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali kuhusu Serikali kupeleka mawasiliano katika Kata husika, inaashiria kuwa bado kuna changamoto. Hivyo, Wizara kupitia UCSAF itafanya tathmini katika kata hiyo ili kubaini mahitaji halisi ya mawasiliano na endapo itabaini kuwepo kwa tatizo la mawasiliano katika kata hiyo ambapo itaingizwa katika zabuni ya miradi itakayotekelezwa katika mwaka wa fedha 2025/2026.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Kata za Magila, Gerezani na Kalalani, Serikali kupitia UCSAF itazifanyia tathmini Kata hizi ili kubaini changamoto za mawasiliano zilizopo na zitajumuishwa katika zabuni zitakazotangazwa katika mwaka wa fedha 2025/2026.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved