Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 15 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 193 | 2025-04-30 |
Name
Atupele Fredy Mwakibete
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busokelo
Primary Question
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Je, lini Barabara inayounganisha Jimbo la Busokelo na Mbeya yenye kilometa 28, itajengwa ili wananchi wasisafiri umbali mrefu kupitia Suma hadi Katumba?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara inayounganisha Jimbo la Busokelo na Mbeya, kupitia Halmashauri ya Busokelo, inajulikana kwa jina la Number One – Lugombo, yenye urefu wa kilometa 30. Barabara hii ni ya Wilaya iliyokasimiwa TANROADS kutoka TARURA mwaka 2023. Serikali imepanga katika mwaka wa fedha 2026/2027 kuanza maandalizi ya kuijenga barabara hii kwa kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili ijengwe kwa kiwango cha lami. Kwa sasa, Serikali inaendelea kuifanyia barabara hii matengenezo ya kawaida ili iweze kupitika katika majira yote ya mwaka.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved