Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 15 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 194 | 2025-04-30 |
Name
Masache Njelu Kasaka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lupa
Primary Question
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE K.n.y. MHE. MASACHE NJELU KASAKA aliuliza:-
Je, lini Selikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya kuanzia Makongolosi hadi Mkiwa?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Makongolosi – Rungwa – Itigi – Mkiwa yenye urefu wa kilometa 413 ni sehemu ya Barabara ya Mbeya – Lwanjilo – Chunya – Makongolosi – Rungwa – Itigi – Mkiwa yenye urefu wa kilometa 524. Ujenzi wa barabara hii unafanyika kwa awamu, ambapo sehemu ya Mbeya hadi Makongolosi, kilometa 111, ujenzi umekamilika. Sehemu ya Noranga – Itigi, Mlongoji, kilometa 25 ujenzi unaendelea na umefikia 76% na sehemu ya Itigi, Mlongoji – Mkiwa, kilometa 31.57, mkandarasi yupo kwenye maandalizi ya kuanza kazi. Kwa sehemu iliyobaki ya kutoka Makongolosi hadi Noranga, kilometa 356.43 Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuendelea na ujenzi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved