Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 15 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 195 | 2025-04-30 |
Name
Suma Ikenda Fyandomo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka magari kwenye vituo vya Polisi Mkoani Mbeya?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi hugawa vitendea kazi kama magari kwa uwiano sawa katika mikoa yote hapa nchini. Katika ugawaji huo pia huzingatia ukubwa wa eneo, wingi wa watu, shughuli za kiuchumi, matukio ya uhalifu na wingi wa makosa ya usalama barabarani. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 Mkoa wa Mbeya umepata magari mapya 12, hivyo kufanya kuwa na jumla ya magari 43 yanayofanya kazi. Serikali itaendelea kutenga fedha toka kwenye bajeti kila mwaka kwa ajili ya kununulia vitendea kazi kwa ajili ya Jeshi la Polisi ikiwemo magari. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved