Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 178 | 2025-02-11 |
Name
Anna Richard Lupembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nsimbo
Primary Question
MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Chumba cha Upasuaji katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ilipokea jumla shilingi bilioni 2.94 na kujenga majengo 12 ya hospitali ya wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, Serikali itatenga shilingi milioni 265 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la upasuaji katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved