Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 179 | 2025-02-11 |
Name
Emmanuel Adamson Mwakasaka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tabora Mjini
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaipatia ufumbuzi changamoto ya upungufu wa vifaa tiba na watumishi kwenye baadhi ya vituo vya afya nchini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba pamoja na kuajiri na kuwapangia vituo vya kazi wataalam wa kada mbalimbali za afya katika ngazi ya msingi kote nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2022/2023 na 2023/2024, Serikali ilitoa shilingi bilioni 187.37 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba ngazi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali za halmashauri. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2024/2025, Serikali imetenga shilingi bilioni 66.7 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na hadi kufikia Disemba, 2024 jumla ya shilingi bilioni 43.13 zimetolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia imeendelea kuajiri wataalam wa kada za afya ambapo katika kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2023/2024, jumla ya wataalam wa kada za afya 25,917 wameajiriwa na kupangiwa vituo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Serikali itaendelea kutoa vibali vya ajira na kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved