Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 180 | 2025-02-11 |
Name
Athumani Almas Maige
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tabora Kaskazini
Primary Question
MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:-
Je, lini Serikali itakipatia Gari la Wagonjwa Kituo cha Afya cha Upuge – Uyui?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuimarisha huduma za rufaa za wagonjwa, ambapo katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2024/2025 Serikali imenunua na kusambaza magari 382 ya kubebea wagonjwa kwenye halmashauri kwa kuzingatia mahitaji, ambapo kila jimbo limepokea angalau gari moja la kubebea wagonjwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Uyui ilipokea magari matatu ya kubebea wagonjwa ambayo yamepangwa kutoa huduma katika Hospitali ya Wilaya, Kituo cha Afya Igalula na Loya. Aidha, Kituo cha Afya Upuge - Uyui kina gari la wagojwa ambalo ni chakavu hali inayopelekea kuhitaji matengenezo ya mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mpango wa manunuzi wa magari ya wagonjwa na kuyapeleka kwenye vituo vyenye uhitaji zaidi kikiwemo Kituo cha Afya cha Upuge – Uyui, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved