Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Finance | Wizara ya Fedha | 183 | 2025-02-11 |
Name
Aloyce John Kamamba
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Buyungu
Primary Question
MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kuweka Kituo cha Forodha katika Kijiji cha Muhange, Nyabibuye na Malenga ili kuongeza kipato kupitia forodha mipakani?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa Serikali inatatua changamoto ya kukosekana kwa huduma za kiforodha katika Vijijiji vya Muhange, Nyabibuye na Malenga imepeleka Maafisa wa Forodha wawili eneo la Muhange kwa ajili ya huduma za forodha. Maafisa wanaohudumia Kituo cha Nyaronga wataanza kuhudumia Nyabibuye kwa awamu kabla ya kufungua ofisi ya huduma na eneo la Malenga litahudumiwa na maafisa kutoka Muhange.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved