Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 185 | 2025-02-11 |
Name
Fatma Hassan Toufiq
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza:-
Je, wananchi wangapi wamepoteza maisha kutokana na ajali za pikipiki kati ya mwaka 2022 hadi 2024?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2022-2024 jumla ya wananchi 1,113 wamepoteza maisha kutokana na ajali zilizosababishwa na pikipiki kwa mchanganuo ufuatao: madereva wa pikipiki waliopata ajali na kufariki ni 759; abiria waliopanda pikipiki na kupata ajali zilizosababisha vifo vyao ni 283; na wananchi waliokuwa wanatembea kwa miguu kandokando ya barabara au njiani, ama waliokuwa wanavuka barabara na kupata ajali ya kugongwa na pikipiki na kufariki dunia ni 71.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa wito kwa madereva wote wanaoendesha pikipiki kuzingatia sheria ya usalama barabarani ili kupunguza ajali zinazoathiri wananchi wengi na kupunguza nguvu kazi katika Taifa letu, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved