Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 186 | 2025-02-11 |
Name
Aziza Sleyum Ally
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AZIZA S. ALLY aliuliza:-
Je, lini Serikali itarudisha Somo la Domestic Science katika Mtaala wa Elimu ya Shule za Msingi Nchini?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, somo la sayansi kimu (domestic science) lilianzishwa baada ya mitaala kubadilishwa mwaka 1979 kufuatia Azimio la Musoma ikiwa ni kutekeleza kauli mbiu ya siasa ni kilimo na elimu kwa wote. Somo hili la sayansi kimu liliboreshwa zaidi na maudhui yake kuingizwa katika somo jipya la stadi za kazi mwaka 1997.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ilikuwa ni pamoja na kupunguza wingi wa masomo kutoka masomo 13 hadi masomo saba kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mtaala ulioboreshwa mwaka 2023 maudhui yanayoshabihiana na somo la sayansi kimu yameboreshwa zaidi kwa kuzingatia mahitaji ya jamii, kukua kwa sayansi na teknolojia pamoja na soko la ajira. Hivyo, maudhui hayo kwa ngazi ya elimu ya msingi yapo kwenye somo la sanaa na michezo, ambalo ni somo la lazima na linafundishwa kuanzia darasa la tatu hadi la sita. Aidha, kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne kuna mkondo maalum unaofundishwa masuala ya chakula na lishe ambao umejikita kuendelea kujenga maarifa katika eneo hili. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved