Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 188 | 2025-02-11 |
Name
Husna Juma Sekiboko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza:-
Je ni lini Serikali itaanzisha Mfuko Maalum wa Mikopo ya Elimu ya Juu (Revolving Fund) ili kuongeza idadi ya wanufaika?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu inatolewa na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu iliyoanzishwa mahsusi kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wa Kitanzania wenye uhitaji na wanaostahili kupata mikopo na ruzuku ili kumudu gharama za masomo ya elimu ya juu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa inatumia fedha zinazokusanywa kutoka kwa warejeshaji walionufaika kama Mfuko wa Mzunguko ili kuwezesha wanafunzi wenye uhitaji waweze kupata mikopo. Hata hivyo, Serikali ipo katika mpango wa kufanya mapitio ya kina (comprehensive review) ya Bodi ya Mikopo ili kuwezesha wahitimu walionufaika kurejesha mikopo yao kwa urahisi. Mapitio haya yakikamilika yataimarisha mifumo ya urejeshaji mikopo na kuifanya Bodi ya Mikopo kuwa stahimilivu katika kujiendesha na kuongeza mapato pamoja na kuongeza idadi ya wanufaika kila mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved