Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 189 | 2025-02-11 |
Name
Joseph George Kakunda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Primary Question
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-
Je, lini Serikali itamaliza tatizo la laini za simu za TTCL kutumika zaidi kutapeli wananchi?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha tatizo la matumizi mabaya ya laini za simu, ikiwemo laini za TTCL, linamalizika. Hatua hizo ni pamoja na:-
(i) Usajili wa laini kwa alama za vidole. Mfumo wa usajili wa laini kwa alama za vidole umelenga kudhibiti laini za simu zinazotumika kwa udanganyifu kwa kuhakikisha kila laini inahusishwa moja kwa moja na mmiliki wake halali;
(ii) Kufuatilia na kufungia laini zinazotumika kwa uhalifu. Serikali kupitia TCRA imeweka mifumo ya kufuatilia matumizi ya laini za simu na kuzifungia zile zinazobainika kutumika kwa ulaghai;
(iii) Kutoa elimu kwa umma. Serikali na wadau mbalimbali wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu jinsi ya kutambua ujumbe wa kitapeli na kuripoti matukio hayo kupitia namba 15040; na
(iv) Ushirikiano na watoa huduma za mawasiliano. TTCL na watoa huduma wengine wanashirikiana na Serikali kuhakikisha kuwa, laini zinazotumika kwa ulaghai zinadhibitiwa mara moja.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved