Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 190 | 2025-02-11 |
Name
Innocent Sebba Bilakwate
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyerwa
Primary Question
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa Barabara ya Omugakorongo – Kigarama hadi Murongo utaanza baada ya kutangazwa upya?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni ya ujenzi wa Barabara ya Omugakorongo – Kigarama – Murongo (kilometa 110); Sehemu ya Murongo hadi Businde kilometa 53.4 imetangazwa upya baada ya zabuni ya awali kukosa Wakandarasi wenye sifa. Zabuni mpya ilitangazwa tarehe 6 Oktoba, 2024 na kufunguliwa tarehe 12 Desemba, 2024. Kwa sasa kazi ya uchambuzi wa zabuni inaendelea na inatarajiwa kukamilika katikati ya mwezi Februari, mwaka huu wa 2025 na baadaye hatua za kumkabidhi mkandarasi zitaendelea. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved