Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 191 | 2025-02-11 |
Name
Joseph Michael Mkundi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Primary Question
MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-
Je, ni hatua ipi imefikiwa na Serikali kuanza ujenzi wa Daraja la Kisorya – Lugezi linalounganisha Wilaya ya Ukerewe na Bunda?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kwa ajili ya Daraja la Kisorya – Lugezi na Barabara unganishi ya Nansio – Rugezi yenye urefu wa kilometa 11. Ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara unganishi kutoka Nansio hadi Rugezi, yenye urefu wa kilometa saba umeanza mwezi Februari, 2024. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha, kwa ajili ya kuanza ujenzi wa daraja. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved