Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 192 | 2025-02-11 |
Name
Mashimba Mashauri Ndaki
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Magharibi
Primary Question
MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanzisha Mfuko wa kuimarisha bei za mazao, ili kusaidia wakulima wa pamba na mazao mengine bei inaposhuka?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa kilimo imeanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo kupitia Tangazo la Serikali, Na. 22 la Tarehe 20 Januari, 2023, baada ya kuidhinishwa na Waziri wa Fedha. Mfuko huo umelenga kuchochea ukuaji wa maendeleo ya Sekta ya Mazao ya Kilimo, kupunguza ukali wa bei ya mazao inaposhuka, kutoa ruzuku ya pembejeo za kilimo (mbegu bora, mbolea pamoja na viuatilifu), kuchochea uwekezaji katika shughuli za utafiti wa kilimo na kuwajengea uwezo wakulima, wasindikaji, Maafisa Ugani na watafiti wa kilimo. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved