Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 18 Sitting 11 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 194 2025-02-11

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:-

Je, lini Bandari ya Kwala itaanza kutumika kwa uhakika Kibaha Vijijini?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) imekamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa Bandari Kavu ya Kwala. Miradi mbalimbali imetekelezwa na kukamilika ikiwemo ujenzi wa reli mchepuko yenye urefu wa kilometa 1.3, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha zege yenye urefu wa kilometa 15.5 kutoka eneo la Kwala hadi Barabara Kuu ya Morogoro, ujenzi wa uzio wa eneo lenye ukubwa wa hekta 60, ambapo kati ya hizo hekta tano zimewekwa sakafu ngumu (pavements), kwa ajili ya kuweza kupokea makasha 3,500 kwa wakati mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamilika kwa awamu ya kwanza ya utekelezaji wa Mradi wa Bandari Kavu ya Kwala, kumeiwezesha bandari hii kuanza kutumika rasmi kuanzia mwezi Agosti 2023, ambapo hadi mwezi Disemba, 2024 jumla ya makasha 684 yamepokelewa. Kati ya hayo, makasha 406 yamekwishakabidhiwa kwa wateja.