Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 18 Sitting 11 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 195 2025-02-11

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-

Je, lini mnara wa mawasiliano wa kuongozea ndege utajengwa katika Uwanja wa Ndege Mpanda?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ili Kiwanja cha Ndege kiwe na mnara wa kuongozea ndege kinahitaji kukidhi matakwa makubwa manne ambayo ni kuwa na ndege za ratiba maalum, kuwa na idadi kubwa ya miruko na mituo ya ndege, kuwa katika eneo lenye hali mbaya ya hewa hasa ambayo inaleta uono hafifu kwa rubani na sababu nyingine za msingi kama itakavyoonekana inafaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivi sasa Kiwanja cha Ndege Mpanda hakijaweza kukidhi matakwa yaliyoainishwa na hivyo huduma za kuongoza ndege zinazotua katika kiwanja hicho hutolewa kutokea mnara uliopo katika Kiwanja cha Ndege cha Tabora kama ilivyokasimiwa na kituo kikuu cha kuongozea ndege kilichopo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.