Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 11 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 195 | 2025-02-11 |
Name
Sebastian Simon Kapufi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpanda Mjini
Primary Question
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-
Je, lini mnara wa mawasiliano wa kuongozea ndege utajengwa katika Uwanja wa Ndege Mpanda?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ili Kiwanja cha Ndege kiwe na mnara wa kuongozea ndege kinahitaji kukidhi matakwa makubwa manne ambayo ni kuwa na ndege za ratiba maalum, kuwa na idadi kubwa ya miruko na mituo ya ndege, kuwa katika eneo lenye hali mbaya ya hewa hasa ambayo inaleta uono hafifu kwa rubani na sababu nyingine za msingi kama itakavyoonekana inafaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivi sasa Kiwanja cha Ndege Mpanda hakijaweza kukidhi matakwa yaliyoainishwa na hivyo huduma za kuongoza ndege zinazotua katika kiwanja hicho hutolewa kutokea mnara uliopo katika Kiwanja cha Ndege cha Tabora kama ilivyokasimiwa na kituo kikuu cha kuongozea ndege kilichopo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved