Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 22 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 276 | 2025-05-12 |
Name
Minza Simon Mjika
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka magari ya wagonjwa katika Vituo vya Afya Iramba Ndogo na Mwasengela - Meatu?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya za dharura na rufaa kwa kununua magari ya wagonjwa na kuyapeleka katika vituo vya huduma za afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024, halmashauri ya Wilaya ya Meatu imepokea magari matatu ya kubebea wagonjwa na kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Meatu, ambapo magari mawili ya kubebea wagonjwa ya Kituo cha Afya Iramba Ndogo na Kituo cha Afya Mwasengela yameachwa katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu kwa muda na pindi majengo ya kutolea huduma za upasuaji wa dharura yatakapokamilika magari hayo yatapelekwa kwenye vituo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved