Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 22 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 284 | 2025-05-12 |
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:-
Je, kuna sera za Vipaumbele kwa ajili ya wanawake wajasiriamali katika miradi ya serikali?
Name
Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkoani
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI K.n.y. WAZIRI WA UCHUKUZI: alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Uchukuzi ya Mwaka 2003 imetoa kipaumbele cha kutambua na kutatua changamoto mbalimbali za wanawake katika kuleta usawa katika jamii. Kwa kupitia Miradi ya Usafirishaji inayotekelezwa na Serikali, wanawake wajasiriamali wamepewa nafasi za kuwezeshwa kufanya biashara katika Vituo vya Reli ya SGR Dar es Salaam – Dodoma. Pia, vituo vya mabasi ya Mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha na Mikoa mingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake wajasiriamali ambao ni madereva wa vyombo vya usafiri wanatoa huduma za usafiri katika vituo hivyo na maeneo ambayo miradi ya Serikali inaendelea kutekelezwa ambapo wamethibitishwa na kusajiliwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA). Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved