Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 22 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 288 | 2025-05-12 |
Name
Florent Laurent Kyombo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkenge
Primary Question
MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoma – Bukwali yenye urefu wa kilometa 35 utakamilika?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza maandalizi, kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami Barabara ya Katoma – Bukwali, yenye urefu wa kilometa 35, kwa kuanza kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kazi hiyo ilianza Machi 2024 na inatarajiwa kukamilika Septemba 2025. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha, kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved