Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 290 | 2025-05-13 |
Name
Dr. Alfred James Kimea
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Korogwe Mjini
Primary Question
MHE. ANNA R. LUPEMBE K.n.y. MHE. ALFRED J. KIMEA aliuliza:-
Je, lini Serikali itazipandisha hadhi Sekondari za Ngombezi, Joel Bendera na Kwamndolwa, Korogwe TC, kuwa za kidato cha tano na sita?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule za Sekondari Ngombezi, Joel Bendera na Kwamndolwa ni shule zilizo kwenye mpango wa kupandishwa hadhi na kuwa za Kidato cha Tano na Sita. Shule hizi zimejengewa baadhi ya miundombinu kwa ajili ya wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita. Hivyo, shule hizi zitapandishwa hadhi pindi zitakapokidhi vigezo. Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ili kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita katika Shule za Sekondari Ngombezi, Joel Bendera na Kwamndolwa kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved