Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 292 | 2025-05-13 |
Name
Husna Juma Sekiboko
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya cha kimkakati kwenye Kata ya Lukozi – Lushoto?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetenga shilingi bilioni 53.5 kupitia Bajeti ya Nyongeza ya mwaka wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya 214 katika Kata za Kimkakati kote nchini ikiwemo Kata ya Lukozi katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto. Kata ya Lukozi imetengewa shilingi milioni 250 na tayari Serikali imeanza kupeleka fedha hizo kwa awamu ya kwanza katika majimbo 120.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved