Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 293 | 2025-05-13 |
Name
Ally Mohamed Kassinge
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilwa Kusini
Primary Question
MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka gari la kubeba wagonjwa katika Kituo cha Afya Nanjirinji Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya vipaumbele muhimu vya Serikali katika kuboresha huduma za afya ni magari ya wagonjwa na magari ya usimamamizi wa huduma za afya. Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 ilinunua magari 594 na kuyapeleka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ilipelekewa magari matatu ya kubebea wagonjwa na kupelekwa Hospitali ya Kinyonga, Kituo cha Afya Chumo na Njinjo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa kwa ajili ya vituo vya afya vyenye uhitaji kote nchini, kikiwemo kituo cha afya Nanjirinji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved