Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Good Governance | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 294 | 2025-05-13 |
Name
Eng. Stella Martin Manyanya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nyasa
Primary Question
MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -
Je, lini Serikali itawalipa watumishi wastaafu waliopandishwa madaraja kisha hatua hizo kusitishwa?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa watumishi ambao walipandishwa vyeo na barua zao za kupandishwa vyeo kuingizwa kwenye Mfumo wa Taarifa za Utumishi na Mishahara na baadaye upandishwaji vyeo huo kusitishwa mwezi Juni, 2016 ili kupisha zoezi la uhakiki. Kundi hili linajumuisha pia watumishi waliostaafu kazi kabla ya Serikali kuruhusu tena upandishaji wa vyeo kuanzia mwezi Novemba, 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia hatua hiyo, Serikali iliridhia na kuelekeza kuwa watumishi waliostaafu kwa aina hiyo, ambao wanastahili kulipwa madai ya malimbikizo ya mishahara ya kuanzia walivyopandishwa vyeo vyao hadi tarehe walipostaafu kazi, walipwe madai yao ya malimbikizo ya mishahara. Aidha, malipo ya madai haya yamekuwa yakifanywa na Serikali kwa wastaafu hawa kupitia kwa waliokuwa waajiri wao, nakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved