Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 296 | 2025-05-13 |
Name
Tunza Issa Malapo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -
Je, kuna mkakati gani wa kuunganisha gesi kwa ajili ya kupikia kwa Taasisi na nyumba za wananchi Mkoani Mtwara?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Mtwara, Serikali imeshapeleka miundombinu ya usambazaji gesi asilia katika baadhi ya maeneo ambapo jumla ya nyumba 425 na taasisi nne zimeunganishwa na mtandao wa matumizi ya gesi asilia katika maeneo ya Mtwara Mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, Serikali kupitia TPDC ipo katika mpango wa kuunganisha nyumba zaidi ya 865 katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mtwara ambapo kuna miundombinu ya bomba la gesi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved