Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 297 | 2025-05-13 |
Name
Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vwawa
Primary Question
MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -
Je, upi mkakati wa Serikali wa kujenga minara ya simu kwenye Kata ya Ipunga, Nyimbili na Isalalo ili kuboresha mawasiliano?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Nyimbili kuna minara miwili iliyojengwa kwa ruzuku ya Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF). Mnara wa kwanza ni wa Kampuni ya Honora (Yas) ambayo ilikuwa TIGO na Mnara wa pili ni wa Kampuni ya Vodacom na minara hii yote imekamilika na inatoa huduma kikamilifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Kata ya Ipunga na Isalalo bado hazijapata fursa ya kunufaika na miradi ya Serikali ya kuboresha huduma za Mawasiliano, hivyo kupitia UCSAF, Kata hizi zitafanyiwa tathmini ili kubaini changamoto za mawasiliano ya simu katika maeneo tajwa na kubaini mahitaji halisi na kuyaingiza katika zabuni zitakazotangazwa kulingana na upatikanaji wa fedha hususan katika mwaka wa fedha 2025/2026. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved