Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 298 | 2025-05-13 |
Name
Joseph Michael Mkundi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Primary Question
MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: -
Je, lini ujenzi wa kivuko cha abiria kutoka Kakukuru kwenda Gana – Ukerewe kitaanza kujengwa?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia wakala wa ufundi na umeme TEMESA katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 inaendelea na utekelezaji wa miradi ya ujenzi na ukarabati wa vivuko mbalimbali nchini. Aidha, baada ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa daraja la JPM, yaani pale Kigongo Busisi Mkoani Mwanza, vivuko vinavyotoa huduma katika eneo hilo vitagawanywa katika maeneo yenye uhitaji wa vivuko katika Mkoa wa Mwanza ikiwa ni pamoja na Kakukuru, kwenda Gana Wilayani Ukerewe. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved