Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Finance and Planning | Wizara ya Fedha | 299 | 2025-05-13 |
Name
Oran Manase Njeza
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbeya Vijijini
Primary Question
MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -
Je, Serikali imewezesha miradi mingapi kwa utaratibu wa ubia wa Serikali na Sekta Binafsi?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 10A cha Sheria ya PPP Sura Na.103 kilianzisha Mfuko wa Uwezeshaji Ubia kwa lengo la kuziwezesha Mamlaka za Serikali kuandaa na kutekeleza miradi ya PPP. Aidha, Kifungu cha 5(1) cha Sheria hiyo imekipa Kituo cha Ubia (PPP Centre) jukumu la kutoa usaidizi wa kiufundi kwa Mamlaka za Serikali na Sekta Binafsi wakati wa uibuaji, maandalizi na utekelezaji wa miradi ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP). Hadi Aprili, 2025 jumla ya miradi 80 imewezeshwa na Serikali, na ipo katika hatua mbalimbali kama ifuatavyo: -
(i) Miradi mitatu ipo katika hatua ya utekelezaji;
(ii) Miradi minne ipo katika hatua ya majadiliano;
(iii) Miradi miwili ipo katika hatua ya ununuzi;
(iv) Miradi 26 ipo katika hatua ya upembuzi yakinifu;
(v) Miradi 13 ipo katika hatua ya upembuzi yakinifu wa awali; na
(vi) Miradi 32 ipo katika hatua ya andiko dhana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved