Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 23 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 301 | 2025-05-13 |
Name
Amina Ali Mzee
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kujumuisha Mada ya ukatili wa kijinsia kwenye Masomo kuanzia Shule za Msingi nchini?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya maboresho ya mitaala katika ngazi za Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Ualimu mwaka 2023 ili kuhakikisha kuwa mitaala yetu inaendana na Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014, Toleo la 2023.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mitaala iliyoboreshwa, ukatili wa kijinsia pamoja na masuala mengine mtambuka yamechopekwa katika masomo mbalimbali katika ngazi zote za elimu. Aidha, somo jipya la Historia ya Tanzania na Maadili ambalo ni somo la lazima kwa wanafunzi wote kuanzia elimu ya Awali mpaka Kidato cha Sita lina mada mahususi zinazolenga kujenga umahiri wa mwanafunzi katika kuelewa na kupinga ukatili wa kijinsia.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved