Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 71 2016-02-02

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:-
Yamekuwepo malalamiko mengi ya kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu wa kupiga watu, kuwatesa, kuchoma mali na kutishia amani katika Kisiwa cha Unguja Wilaya za Magharibi na Mjini na kwamba wahusika wamekuwa hawajulikani:-
(a) Je, ni kwanini hali hiyo imeachwa kuendelea kwa muda mrefu?
(b) Je, ni kwa nini Jeshi la Polisi limeshindwa kuwakamata wahusika?
(c) Je, wananchi hao wategemee lini vitendo hivyo kutoweka?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Saleh Ally, Mbunge wa Malindi, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kulikuwepo na ongezeko la matukio saba ya uhalifu katika Wilaya ya Magharibi na Mjini kwa mwaka 2015 ambapo jumla ya matukio 139 yaliripotiwa katika Vituo vya Polisi ikilinganishwa matukio 132 ya mwaka 2014. Hata hivyo pamoja na kuwepo kwa ongezeko hilo takwimu zinaonesha kuwa vitendo hivyo vya makosa ya jinai kwa ujumla Visiwani Zanzibar vinapungua kwa kasi ya kuridhisha. Mathalani, kwa mwaka 2015 jumla ya makosa 1,673 ya jinai yaliripotiwa katika Kituo cha Polisi, ikilinganishwa na makosa 3,227 yaliyoripotiwa mwaka 2014. Hii ni pungufu ya makosa 1,554, sawa na wastani wa asilimia 51.8.
Mheshimiwa Naibu Spika, vitendo vya uhalifu Zanzibar havijafumbiwa macho hata kidogo kama inavyodhaniwa na baadhi ya watu, kwani kutokana na takwimu zilizoainishwa awali, ni dhahiri kuwa uhalifu Zanzibar sio tu wa kutisha na unaendelea kudhibitiwa. Jeshi la Polisi linao wataalam wa kupambana na wahalifu wa aina mbalimbali na litaendelea kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wale wote wanaovunja sheria.