Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 6 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 54 2016-11-07

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIUS F. NGALAWA aliuliza:-
Pamoja na kwamba Jimbo la Ludewa lina vyanzo vingi vya maji, lakini kuna matatizo makubwa sana ya maji na wadau mbalimbali wamekuwa wakijitokeza kusaidia tatizo hili lakini Serikali na Halmashauri zimekuwa hazitoi ushirikiano kwa kurudi nyuma katika kuchangia sehemu yao kwa kigezo cha kutokuwa na fedha. Mfano vijiji vya Maholongwa, Mlangali, Mavanga, Manda, Nkomang’ombe na Lwela.
(a) Je, Serikali iko tayari kuweka kipaumbele katika kusaidia pale inapohitajika kuchangia?
(b) Je, nini kauli ya Serikali katika kushughulikia tatizo la maji Jimboni Ludewa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deogratius Francis Ngalawa, Mbunge wa Ludewa lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miradi ya maendeleo unafanyika kwa njia shirikishi yaani Serikali, wadau wa maendeleo na wananchi kupitia mpango wa fursa na vikwazo kwa maendeleo. Kwa utaratibu huo mafanikio makubwa yamepatikana katika kuboresha huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, Serikali imeweka kipaumbele na kutenga shilingi milioni 861 kwa ajili ya kukamilisha mradi wa maji katika Kijiji cha Lugarawa, ukarabati wa miradi ya maji Lifua/Manda na Kijiji cha Ludewa K. Vilevile Serikali inashirikiana na taasisi isiyo ya Kiserikali ya Lusala Development Association kwa ajili ya kukamilisha mradi wa maji katika vijiji vya Mlangali, Mavanga na Nkomang’ombe utakaogharimu shilingi milioni 250 ambapo mchango wa Serikali ni shilingi milioni 50.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inapongeza mchango mkubwa wa wadau mbalimbali kushirikiana na wadau wa maendeleo katika sekta za maji zikiwemo taasisi za dini. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo na kuhakikisha bajeti inatengwa kila mwaka kwa ajili ya kutatua tatizo la maji kwa wananchi wa Ludewa na maeneo mengine hapa nchi.