Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIUS F. NGALAWA aliuliza:- Pamoja na kwamba Jimbo la Ludewa lina vyanzo vingi vya maji, lakini kuna matatizo makubwa sana ya maji na wadau mbalimbali wamekuwa wakijitokeza kusaidia tatizo hili lakini Serikali na Halmashauri zimekuwa hazitoi ushirikiano kwa kurudi nyuma katika kuchangia sehemu yao kwa kigezo cha kutokuwa na fedha. Mfano vijiji vya Maholongwa, Mlangali, Mavanga, Manda, Nkomang’ombe na Lwela. (a) Je, Serikali iko tayari kuweka kipaumbele katika kusaidia pale inapohitajika kuchangia? (b) Je, nini kauli ya Serikali katika kushughulikia tatizo la maji Jimboni Ludewa?

Supplementary Question 1

MHE. DEOGRATIUS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini bado tunauliza. Wadau mbalimbali wamekuwa wakichangia michango hii ya maji kwa karibu sana lakini Serikali imekuwa ikusuasua kupeleka hizi hela.
Je, Mheshimiwa Waziri ananithibitishiaje kwamba tutazipata fedha hizi kwa haraka?
Pili, kwa sababu wadau wa maendeleo wamekuwa wakileta ile michango na kazi inakuwa imeshafanyika, kutokana na Serikali kuchelewesha michango yao inakuta kwamba baadhi ya miundombinu inakuwa tayari imeshabomoka.
Je, Serikali inaweza ikagharamia ile miundombinu iliyobomoka kwa sababu ya kucheleweshwa kwa fedha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS-TAMISEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumze wazi kwa sababu Serikali kuna commitment ya shilingi milioni 50, na kwa sababu jukumu letu kubwa ni kuhakikisha miradi ya maji iliyotengwa katika kipindi hichi inaweza ikapata msaada wa haraka. Naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Deogratius, ofisi yetu itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha tunasukuma pesa hii milioni 50, kama ni matching grands ya kuhakikisha mradi huo unatekelezeka, tutaweza kulifanya hili wala usihofu, mimi mwenyewe naomba nitoe commitment hiyo kama Serikali kuhakikisha jambo hili linakaa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima kwamba miradi mingine imetekelezwa lakini mpaka imechakaa. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhakikisha miradi ile sasa inarekebishwa kuweza kufanyakazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Deo kuwa tutakachokifanya kwanza ofisi yetu itawasiliana na Ofisi wa RAS Mkoa wa Njombe, kuangalia ni jinsi gani kama kuna miradi ambayo ina changamoto kubwa na kubainisha ni kitu gani kinatakiwa kifanyike. Kwa sababu mwisho wa siku, mradi kama umetekelezwa lakini mradi saa nyingine umeharibika kabla ya kuwapatia wananchi fursa hiyo ya maji ina maana tutakuwa hatujafikia malengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Ofisi ya RAS Mkoa wa Njombe naomba niiagize kupitia mkutano huu, kwamba wahakikishe wanafanya follow up katika Jimbo hili la Ludewa kuangalia changamoto iliyokuwepo halafu tuangalie mkakati sasa, tutafanyaje ili mradi miradi hiyo iweze kufanya kazi. Lengo kubwa wananchi wako Mheshimiwa Deo waweze kupata fursa ya maji, na hiyo ndio azma ya Serikali kwamba kuhakikisha inawahudumia wananchi wake.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. DEOGRATIUS F. NGALAWA aliuliza:- Pamoja na kwamba Jimbo la Ludewa lina vyanzo vingi vya maji, lakini kuna matatizo makubwa sana ya maji na wadau mbalimbali wamekuwa wakijitokeza kusaidia tatizo hili lakini Serikali na Halmashauri zimekuwa hazitoi ushirikiano kwa kurudi nyuma katika kuchangia sehemu yao kwa kigezo cha kutokuwa na fedha. Mfano vijiji vya Maholongwa, Mlangali, Mavanga, Manda, Nkomang’ombe na Lwela. (a) Je, Serikali iko tayari kuweka kipaumbele katika kusaidia pale inapohitajika kuchangia? (b) Je, nini kauli ya Serikali katika kushughulikia tatizo la maji Jimboni Ludewa?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi ili kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shida ya maji katika Jimbo la Ludewa inafanana sana na shida ya maji katika Jimbo la Ukonga. Ukitembelea kata za Kivule, Msongola, Chanika, Buyuni, Zingiziwa, Pugu, Pugu Station, Ukonga, Gongo la Mboto na Kipunguni. Kata hizi zote hazina maji kabisa na hasa maji ambayo yanasimamiwa na Serikali ambayo ni maji safi na salama.
Sasa nilikuwa naomba kuuliza, kwa sababu nimezungumza mara nyingi Bungeni hapa kuuliza shida ya maji Dar es Salaam na hasa Jimbo la Ukonga ni nini kauli ya Serikali na hasa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana kwamba baada ya Bunge hili tuongozane kwenda Ukonga akashuhudie watu wa Ukonga wanavyokunywa maji machafu na hasa kwenye shule, zahanati na vituo vya afya?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Jimbo la Ukonga lina changamoto ya upatikanaji wa maji. Lakini tunayo mipango ambayo inayoendelea katika Mpango wa Utekelezaji wa Programu Phase II ipo miradi ambayo Jimbo la Ukonga wametengewa fedha. Lakini katika mpango wa muda mrefu, maeneo ya Ukonga, Mkaranga na maeneo ya Kigamboni, maji yatapatikana kutoka chanzo cha Mpera na Kimbiji. Ambapo sasa utekelezaji wake tumeanza kuchimba visima karibu visima 20 vinakamilika. Baada ya hapo tunajenga miundombinu ambayo tutapeleka maeneo hayo ya Ukonga na kutakuwa hakuna tatizo kubwa na nikuahidi kwamba katika kipindi cha miaka hii minne ambayo imebakia katika Seriali ya Awamu ya Tano, tutahakikisha kwamba Ukonga inakuwa na maji ya kutosha.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEOGRATIUS F. NGALAWA aliuliza:- Pamoja na kwamba Jimbo la Ludewa lina vyanzo vingi vya maji, lakini kuna matatizo makubwa sana ya maji na wadau mbalimbali wamekuwa wakijitokeza kusaidia tatizo hili lakini Serikali na Halmashauri zimekuwa hazitoi ushirikiano kwa kurudi nyuma katika kuchangia sehemu yao kwa kigezo cha kutokuwa na fedha. Mfano vijiji vya Maholongwa, Mlangali, Mavanga, Manda, Nkomang’ombe na Lwela. (a) Je, Serikali iko tayari kuweka kipaumbele katika kusaidia pale inapohitajika kuchangia? (b) Je, nini kauli ya Serikali katika kushughulikia tatizo la maji Jimboni Ludewa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mradi wa maji ni tatizo kweli, katika Wilaya ya Morogoro Vijijini, katika vijiji vya Furwe, Mikese, Gwata waliahidiwa mradi wa maji kwa muda wa miaka mingi, na wananchi wanateseka kwa maji kwa muda mrefu. Je, naomba kuuliza wananchi hawa ambao wameteseka kwa muda na wameahidiwa mradi wa maji watapata lini maji na mradi huu utatekelezwa lini?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshatoa maelekezo katika kila Halmashauri namna ya kupanga vipaumbele katika vijiji ambavyo havina maji; sasa awamu hii ya kwanza siwezi kusema ni vijiji vipi vimepangwa, lakini Halmashauri yake inafahamu na wameleta vipaumbele na tumeweka kwenye bajeti na fedha zimetengwa. Kwa hiyo, sasa hivi ni ufuatilia tu utekelezaji, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge nitakaa naye ili kusudi niweze kuona hivyo vijiji anavyovisema vipo kwenye mpango wa mwaka huu au vipi, ili tuweze kuona namna ya kufanya.