Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 7 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 78 2016-11-08

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:-
Je, ni nini umuhimu wa kuwa na Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya katika nchi hii?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali namba 78 la Mheshimiwa Salma Mohamed Mwassa, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya hapa nchini yanaundwa na kusimamiwa na kifungu cha 22 cha Sheria ya Mahakama ya Ardhi Namba 2 ya mwaka 2002.
Mheshimiwa Spika, umuhimu wa kipekee wa Mabaraza haya ni suala zima la utatuzi wa migogoro yote itokanayo na matumizi ya ardhi nchini kwa karibu zaidi ukilinganisha na vyombo vingine vya kutatua migogoro. Hivyo, Mabaraza haya yana umuhimu mkubwa sana katika kuleta amani na muafaka katika maeneo mengi yenye migogoro ya watumiaji wa ardhi nchini.
Mheshimiwa Spika, umuhimu mwingine ni kutatua migogoro yote ya ardhi kwa haraka na kwa njia rafiki na shirikishi kwa kuwa Mabaraza haya yako karibu na wananchi wa eneo husika.
Mheshimiwa Spika, umuhimu huu umejidhihirisha katika utendaji wake. Kati ya Oktoba, 2004 mpaka kufikia Oktoba, 2016 jumla ya mashauri 131,470 yalipokelewa na kati yake mashauri 100,744 yameamuliwa na mashauri 32,176 bado yanaendelea.