Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 8 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 82 2016-11-09

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:-
Licha ya kwamba chanzo cha maji yanayotumika katika Manispaa ya Mpanda kipo katika Kijiji cha Ikolongo, Kata ya Mtapenda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, lakini wananchi wa maeneo haya hawapati maji:-
(a) Je, kwa nini Serikali katika bajeti ya mwaka 2016/2017 isitenge fedha ya miradi ya maji ili wananchi wa viiji jirani vya Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambazo ni Kapalala, Itenka, Machimboni, Sitalike, Kanoge na Katumba wapate maji?
(b) Kwa kuwa Mto Ugalla ni chanzo kizuri cha maji: Je, Serikali itaondoa lini kero ya maji katika Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Nsimbo, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, imetenga shilingi milioni 757.4 kwa ajili ya miradi ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo. Miradi iliyopangwa kutekelezwa ni pamoja na upanuzi wa mradi wa Nduwi Station katika Kata ya Ntumba, kujenga mradi wa maji katika Kijiji cha Katisunga, kujenga mradi wa maji katika Kijiji cha Songambele, Kata ya Kapalala pamoja na uchimbaji wa visima virefu sita.
(b) Mheshimiwa Spika, kulingana na tathmini iliyofanywa na Mkoa kupitia Mamlaka ya Maji, Mkoa wa Katavi mwezi Desemba, 2015, chanzo cha Mto Ugalla kimeonekana kuwa siyo cha uhakika kutokana na kupungua kwa maji wakati wa kiangazi. Serikali ina mpango wa kutumia Ziwa Tanganyika ambacho ni chanzo cha uhakika kwa ajili ya kupeleka maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo na Mpanda.