Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Licha ya kwamba chanzo cha maji yanayotumika katika Manispaa ya Mpanda kipo katika Kijiji cha Ikolongo, Kata ya Mtapenda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, lakini wananchi wa maeneo haya hawapati maji:- (a) Je, kwa nini Serikali katika bajeti ya mwaka 2016/2017 isitenge fedha ya miradi ya maji ili wananchi wa viiji jirani vya Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambazo ni Kapalala, Itenka, Machimboni, Sitalike, Kanoge na Katumba wapate maji? (b) Kwa kuwa Mto Ugalla ni chanzo kizuri cha maji: Je, Serikali itaondoa lini kero ya maji katika Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga?

Supplementary Question 1

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Serikali, napenda tu kuiambia Serikali kwamba Halmashauri ya Nsimbo ni moja ya Halmashauri katika nchi yetu ya Tanzania ambayo wananchi kwa kiwango cha chini kabisa wanapata maji safi na salama. Ni asilimia 34 tu. Sasa katika hii bajeti ya milioni 757, kuna miradi ya Kijiji cha Katesunga na Kijiji cha Nduwi ambayo itafadhiliwa na World Bank kama shilingi milioni 273: Je, ni lini fedha hizi zitapatikana ili miradi hii iweze kuanza?
Swali la pili, kutokana na majibu ya Serikali kwamba Mto Ugalla una maji machache kwa kipindi cha kiangazi, lakini wananchi wa pale wamekuwa wakitumia mto ule kwa ajili ya maji kipindi chote na kuna mamba ambao wanahatarisha sana maisha yao: Je, kwa nini Serikali wakati mpango wa muda mrefu; maji kutoa Ziwa Tanganyika ukiwa unafanyika, isitenge fedha ili wananchi wa Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga waweze kupata maji kutoka Mto Ugalla?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali la kwanza kwamba lini fedha zitapatikana; mpango wa upatikanaji wa fedha ni katika mwaka huu wa fedha katika bajeti hii. Ndio maana juzi hapa katika Maswali kwa Waziri Mkuu siku ya Alhamisi, Waziri Mkuu aliongelea suala zima la mtiririko wa fedha na akalihakikishia Bunge hili kwamba kipindi siyo kirefu sana tutaanza kuziona fedha katika Halmashauri zetu; fedha za maendeleo na fedha za OC. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba tuwe na imani kwamba katika mchakato huu wa sasa hivi kabla muda haujapita sana, bajeti hizi zitaanza kutoka ili mradi iweze kutekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, kuhusu Mto Ugalla kwamba kwa nini usitumike kwa sasa, kwa sababu mpango uliokuwepo ni wa muda mrefu? Naomba nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Richard Mbogo ni Mbunge ambaye nilikuwa naye Jimboni kwake Nsimbo na miongoni mwa miradi tuliyoikagua ni miradi ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri wazi kwamba nilivyotembelea Jimbo la Nsimbo, ni kweli shida ya maji imekuwa ni kubwa sana. Kwa hiyo, nadhani hili ni wazo jema. Tutalichukua lakini tutawashirikisha na wenzetu kule katika Halmashauri na katika Mkoa, kuona kama ule mradi mkubwa kutoka Ziwa Tanganyika, huenda una gharama kubwa sana, tujue ni kiasi gani, tuweze kuja na mpango mwingine mbadala kusaidia katika Kata hizi ili tusisubiri muda mrefu sana miaka miwili, mitatu au minne kwa wananchi kuendelea kupata shida ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimwambie Mheshimiwa Richard Mbogo kwamba jambo hili sasa tutalichukua, tuone ni jinsi gani tutafanya ili kama katika hizo Kata mbili kuna mradi mwingine mbadala tuweze kuufanya. Nadhani jambo hili ni jambo shirikishi sana kwetu Serikali na Halmashauri ya Wilaya. Tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua anafuatilia sana ili wananchi katika zile kata mbili wapate fursa ya maendeleo ya maji.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Licha ya kwamba chanzo cha maji yanayotumika katika Manispaa ya Mpanda kipo katika Kijiji cha Ikolongo, Kata ya Mtapenda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, lakini wananchi wa maeneo haya hawapati maji:- (a) Je, kwa nini Serikali katika bajeti ya mwaka 2016/2017 isitenge fedha ya miradi ya maji ili wananchi wa viiji jirani vya Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambazo ni Kapalala, Itenka, Machimboni, Sitalike, Kanoge na Katumba wapate maji? (b) Kwa kuwa Mto Ugalla ni chanzo kizuri cha maji: Je, Serikali itaondoa lini kero ya maji katika Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Lushoto limezungukwa na vyanzo vingi vya maji: Je, Serikali ina mpango gani ya kuwatua ndoo kichwani akinamama hasa wa Kilole, Kwekanga, Mbwei, Makanya, Ngulwi, Ubiri, Kwemakame na maeneo mengine yaliyobaki katika Jimbo la Lushoto?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa maji kwa sasa hivi ambao Waziri wa Maji wakati wote huwa anaelezea hapa, lengo letu kubwa ni kumtua mama ndoo kichwani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Shekilindi, kwamba, katika ratiba yangu kama tulivyoongea, tarehe 24 mwezi huu wa Novemba, nitakuwa katika Jimbo lake la Lushoto. Naomba tukiwa kule kule site tuweze kubadilishana mawazo. Hivyo vyanzo vilivyoko, lakini vile vile na wenzetu Wizara ya Maji ambao Mheshimiwa Waziri wa Maji yuko makini muda wote kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanapata maji, tutaangalia na kushauri vizuri jinsi gani tutafanya kwa maeneo ya Wilaya ya Lushoto ili wananchi waweze kupata maji. Kwa hiyo, naomba tutumie vizuri ziara yetu ya tarehe 24 kuangalia vyanzo vilivyoko na mambo mengine kuwasaidia wananchi wa Lushoto.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Licha ya kwamba chanzo cha maji yanayotumika katika Manispaa ya Mpanda kipo katika Kijiji cha Ikolongo, Kata ya Mtapenda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, lakini wananchi wa maeneo haya hawapati maji:- (a) Je, kwa nini Serikali katika bajeti ya mwaka 2016/2017 isitenge fedha ya miradi ya maji ili wananchi wa viiji jirani vya Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambazo ni Kapalala, Itenka, Machimboni, Sitalike, Kanoge na Katumba wapate maji? (b) Kwa kuwa Mto Ugalla ni chanzo kizuri cha maji: Je, Serikali itaondoa lini kero ya maji katika Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa mradi wa maji unaoendelea Manispaa ya Sumbawanga umechukua muda mrefu na wananchi wa Manispaa ya Sumbawanga mpaka sasa hawajui huo mradi utaisha lini: Je, Serikali inawaambiaje wananchi wa Manispaa ya Sumbawanga ikiwepo wanawake ambao wanapata athari mpaka sasa na wengine kupata vifo kwa ajili ya kufuata maji kwenye umbali mrefu?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali ina mradi mkubwa wa maji pale Manispaa ya Sumbawanga. Mradi ule ulikuwa umalizike toka Septemba, 2015, sasa yalitokea matatizo; kwanza, ilikuwa ni kuchimba visima 12; visima sita virefu upande wa kusini na visima sita upande wa kaskazini. Kwa hiyo, ikabidi baada ya kuanza kuchimba tukakosa, visima vyote havikuwa na maji. Kwa hiyo, tukatafua upande wa Kaskazini, ikabidi tuongeze sasa idadi ya visima kutoka sita mpaka 17, hii ikasababisha muda kuongezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie wananchi wa Sumbawanga, kwanza mradi kwa sehemu kubwa umeshakamilika, kilichobaki ni kujenga mtandao. Ikifika mwezi Desemba mwaka huu mradi ule utakuwa umekamilika na wananchi wa Manispaa ya Sumbawanga watakuwa wanapata maji.

Name

Mbaraka Salim Bawazir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:- Licha ya kwamba chanzo cha maji yanayotumika katika Manispaa ya Mpanda kipo katika Kijiji cha Ikolongo, Kata ya Mtapenda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, lakini wananchi wa maeneo haya hawapati maji:- (a) Je, kwa nini Serikali katika bajeti ya mwaka 2016/2017 isitenge fedha ya miradi ya maji ili wananchi wa viiji jirani vya Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambazo ni Kapalala, Itenka, Machimboni, Sitalike, Kanoge na Katumba wapate maji? (b) Kwa kuwa Mto Ugalla ni chanzo kizuri cha maji: Je, Serikali itaondoa lini kero ya maji katika Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga?

Supplementary Question 4

MHE. MBARAK S. BAWAZIR: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Nataka nimwulize Mheshimiwa Waziri, ni lini atamalizia mradi wa maji wa Kilosa, hasa akizingatia kwamba hivi sasa Kilosa kuna kipindupindu? Imebakia pesa kidogo ili wamalizie mradi huo wa maji endelevu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwenye maji, kwa kweli maji yako mengi sana Kilosa na kuna mabwawa yanahitajika yachimbwe kama Kilimagai, Godegode na Kidete. Haya mabwawa yatasaidia hata kuleta mafuriko ndani Kilosa yangu na vile vile katika…
Duh, ahsante

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirejee pia kwa Waheshimiwa Wabunge wote. Hii miradi ya maji katika mwaka wa fedha 2016/2017 tumeainisha kila Wilaya ni miradi ipi ambayo ni vipaumbele inakwenda kufanywa na fedha zimetengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba sana Mheshimiwa Mbunge aseme specifically ni mradi upi anaoulizia? Kwa sababu ndani ya Kilosa ipo miradi mingi, ili tuweze kujua hasa ni upi na ni hatua gani ambazo tunaweza kuzichukua. Kwa hiyo, naomba tuwasiliane na Mheshimiwa Mbunge, tukae ili tuweze kubadilishana mawazo tuone ni namna gani huo mradi ambao anauulizia, nimpe majibu ambayo ni sahihi.