Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 34 2017-02-02

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:-
Kumekuwa kukitokea taarifa juu ya kuanza kazi ya uchimbaji katika Migodi ya Liganga na Mchuchuma.
(a) Je, ni lini kazi hiyo itaanza?
(b) Je, nini mazao ya migodi hiyo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi unganishi ya Mchuchuma na Liganga inatekelezwa na kampuni ya ubia kati ya NDC na Sichuan Hongda Group Limited ya China inayojulikana kwa jina Tanzania China International Mineral Resources Limited. Kampuni hii imekamilisha uchorongaji na upembuzi yakinifu wa miradi hiyo. Uchorongaji umeonesha kuwepo kwa tani milioni 428 za makaa ya mawe eneo la Mchuchuma na tani milioni 126 za chuma eneo la Liganga. Upembuzi yakinifu umeonesha Mgodi wa Chuma Liganga una uwezo wa kuzalisha tani milioni 2.9 kwa mwaka na Mgodi wa Makaa ya Mawe ulioko Mchuchuma una uwezo wa kuzalisha tani milioni tatu kwa mwaka; lakini pia uwezo wa kufua umeme wa megawati 600.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, gharama za uwekezaji katika miradi hii ni dola za Marekani bilioni tatu ambapo dola bilioni 600 ni mtaji wa mwekezaji na mkopo utakuwa dola bilioni 2.4.
Mheshimiwa Naibu Spika, kampuni imekwishapata leseni maalum za uchimbaji wa chuma na makaa ya mawe kutoka Wizara ya Nishati na Madini pamoja na vibali vya mazingira mbalimbali. Pia imepata maeneo katika eneo la Katewaka pamoja na Mchuchuma na Lupali. Kazi ya uthamini na makazi na mali ya wananchi walio ndani ya maeneo ya miradi wanaotakiwa kupisha shughuli za mradi, zimekamilika na hivi sasa tathmini ya fidia iko kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali ipo katika hatua za mwisho za mazungumzo na mwekezaji. Mradi huu utaanza mara baada ya kukamilisha fidia na wananchi waliopisha mradi pia na Government Notice kwa ajili ya incentive za mradi itakapotolewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hiyo unganishi itawawezesha kuchimba makaa ya mawe kiasi cha milioni tatu na chuma ghafi tani milioni 2.9 kwa mwaka. Aidha, sehemu ya makaa ya mawe itatumika kuzalisha umeme na nyingine kwa ajili ya matumizi ya viwandani. Vilevile sehemu ya chuma itatumika kwenye Sekta ya Ujenzi, Viwanda, Kilimo, na kadhalika, lakini madini ya vanadium yatatumika kwa ajili ya matumizi kwenye viwanda vya kemikali pamoja na magari, lakini kadhalika madini ya titanium kwa ajili ya matumizi kwenye viwanda, ndege, meli, pamoja na magari.