Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Kumekuwa kukitokea taarifa juu ya kuanza kazi ya uchimbaji katika Migodi ya Liganga na Mchuchuma. (a) Je, ni lini kazi hiyo itaanza? (b) Je, nini mazao ya migodi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, imeshajionesha kwamba katika machimbo mbalimbali ya madini, wananchi wanaozunguka maeneo hayo huwa wanaathirika sana na pia wanakuwa hawana shughuli ya kufanya katika ile migodi. Sasa kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Njombe ni wananchi wanaojituma sana kwenye kilimo, je, Serikali iko tayari sasa kuanza mchakato maalum wa kusaidia wananchi wanaozunguka maeneo yale hasa Jimbo la Ludewa na Njombe Mjini, waweze kuwa tayari kuzalisha bidhaa za chakula kitaalam, pindi migodi hii itakapoanza waweze kunufaika na soko litakalokuwepo pale migodini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa namshukuru Mheshimiwa Mwalongo kwa jinsi anavyofuatilia kwa ukaribu suala hili kwa manufaa ya wananchi wa Njombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, juhudi za Serikali zinazochukuliwa kuhakikisha kwamba wananchi wananufaika hasa katika masuala ya local content kwa maana ya ushirikishwaji, Serikali imechukua hatua kadhaa; mojawapo ni pamoja na kuitaka kampuni itakayowekeza kutoa elimu pamoja na mikopo ili kuwawezesha wananchi hao kunufaika na rasilimali hiyo. Katika kazi hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na nimshukuru sana, vijiji vya Itoni pamoja na Nanundu ambayo ipo katika maeneo yale, vimeshapewa elimu kwa ajili ya ulimaji wa mboga mboga, lakini pia katika shughuli za kufuga kuku pamoja na kufuga nguruwe. Kwa hiyo, wananchi wataweza kufanya kazi kwa ajili ya kujiwekeza kiuchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, niongeze tu kwamba Serikali kwa kushirikiana na kampuni, kampuni itaanza kutoa mikopo kwa ajili ya kuwawezesha wananchi wanaozunguka mgodi ule kufanya shughuli ndogo ndogo za kiuwekezaji ili pia sasa waanze kushiriki mara baada ya mradi kuanza kwenye shughuli za kibiashara na za kiuchumi katika maeneo yale. Inatoa elimu, lakini inatoa mikopo ya masharti nafuu ili wananchi waanze kufanya hivyo. Utaratibu huu ulianza tangu Oktoba, 2012 na unaendelea hadi sasa.

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Kumekuwa kukitokea taarifa juu ya kuanza kazi ya uchimbaji katika Migodi ya Liganga na Mchuchuma. (a) Je, ni lini kazi hiyo itaanza? (b) Je, nini mazao ya migodi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda tu kuzungumza hapo kwamba tarehe 19 mwezi wa nne liliulizwa swali kwenye Bunge lako Tukufu kuwa Mradi wa Chuma, Liganga na Makaa ya Mawe Mchuchuma, utaanza lini? Majibu ya Serikali yalikuwa kwamba kwanza fidia italipwa mwezi Juni, 2016 ambayo fidia hiyo haijalipwa mpaka leo na pili miradi hii kwamba itaanza mwezi Machi, 2017.
Je, mkanganyiko huo unatokana na nini na majibu hayo yote ambayo sasa hivi inaonekana hayajitoshelezi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa anavyosema Mheshimiwa Mbunge ni sahihi. Kwenye Bunge la mwezi Aprili tulisema kwamba mradi huu utaanza mapema ifikapo mwezi Machi. Hivi sasa bado tupo Januari, hivyo Mheshimiwa Mbunge nadhani avute subira.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kuhusu suala la fidia; fidia inayotarajiwa kufidiwa wananchi wale inafikia takribani shilingi bilioni 13.34, ni kiasi kikubwa. Kwa hiyo, kinachofanyika sasa ni kupitia tathmini halisi ya fidia hiyo, halafu baada ya zoezi hilo kukamilika, basi wananchi watalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kama ambavyo nimeeleza kwenye jibu langu la msingi kwamba yapo masuala ya kimkataba ambayo Serikali pamoja na mwekezaji inayapitia, likiwemo suala la incentives kwa maana ya vivutio, mara baada ya kukamilika, basi mradi huu utaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni matarajio yetu zoezi hili likikamilika kabla ya mwezi Machi, basi kweli mradi huu utaanza mara moja.