Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 87 2017-02-08

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba za makazi Askari Polisi na Magereza katika Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma?
(b) Je, Serikali imejipangaje kufanya ukarabati kwa nyumba za askari zilizopo Wilayani Tunduru ambazo kwa muda mrefu hazijafanyiwa ukarabati?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa nyumba za makazi, maafisa na askari, Serikali imeendelea na utekelezaji wa mpango wa kujenga nyumba mpya kwenye baadhi ya magereza nchini kwa kutumia fedha zinazotengwa katika fungu la bajeti ya maendeleo kila mwaka. Kwa kutambua uhaba na uchakavu wa nyumba za Askari Polisi na Magereza, Serikali ina mpango wa kuwajengea askari nyumba 9,500 nchi nzima ikiwemo kwenye Gereza la Wilaya ya Tunduru pamoja na nyumba 4,136 kwa upande wa polisi, ikijumuisha Wilaya ya Tunduru.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na tatizo la uchakavu wa nyumba za makazi za maafisa na askari, Serikali itaendelea kuzifanyia ukarabati nyumba za Askari Magereza na Polisi nchini zikiwemo za Wilaya ya Tunduru kwa kutenga bajeti ya ukarabati kwa kila mwaka wa fedha kutegemeana na bajeti itakavyoruhusu.