Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba za makazi Askari Polisi na Magereza katika Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma? (b) Je, Serikali imejipangaje kufanya ukarabati kwa nyumba za askari zilizopo Wilayani Tunduru ambazo kwa muda mrefu hazijafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 1

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza ifahamike kwamba Wilaya nyingi zilizopo Mkoani Ruvuma zipo mpakani, kwa mfano Wilaya ya Nyasa inapakana na Malawi, Wilaya ya Tunduru inapakana na Msumbiji. Kuwa na makazi bora ya polisi katika maeneo haya kutahamasisha polisi wetu kuishi katika makazi salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Mheshimiwa Waziri ameeleza kuna nyumba 9,500 zinategemewa kujengwa nchi nzima. Napenda kujua kati ya nyumba hizo ni ngapi zitajengwa Mkoani Ruvuma?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, pale Wilayani Tunduru kulikuwa na jengo ambalo lilikuwa linatumiwa na Askari Polisi wanapokuja kuhamia, jengo lile liliungua moto. Jengo lile lilikuwa linasaidia sana na hasa kwa askari wa kike kupata makazi pale wanapokuja kuhamia. Naomba kujua Serikali imejipangaje katika kuhakikisha jengo lile linajengwa tena ili liwasaidie askari wale?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na nyumba ngapi zinatarajiwa kujengwa Mkoa wa Ruvuma ni 320.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusiana na jengo hilo ambalo amelizungumza tunachukua concern yake tuone ni hatua gani tutachukua ili kuweza kulifanyia ukarabati ikiwezekana katika bajeti zinazofuata.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba za makazi Askari Polisi na Magereza katika Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma? (b) Je, Serikali imejipangaje kufanya ukarabati kwa nyumba za askari zilizopo Wilayani Tunduru ambazo kwa muda mrefu hazijafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 2

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kule Musoma nako tumekuwa na tatizo kubwa sana la nyumba za askari na kwa bahati nzuri Serikali iilisikia kilio chetu. Hivi ninavyozungumza ni zaidi ya miaka mitatu sasa kuna jengo kubwa la ghorofa ambalo limejengwa pale Musoma Mjini. Cha kushangaza mpaka leo askari wetu hawajakabidhiwa. Nataka kujua Serikali inasubiri nini kukabidhi jengo hilo ili liweze kusaidia kuondoa ile adha kubwa wanayopata maaskari wetu?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

Waheshimiwa Wabunge linapofika suala la maslahi ya askari, robo ya tatu ya Bunge huwa wanasimama kutaka askari wetu wapewe maslahi hayo. Nitakapokuwa nakutana nao nitawaambia kwamba Wabunge huwa wanawasemea ili mnapopita majimboni wawape ushirikiano. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu jengo la Mara, kuna hatua za ukamilishwaji ambazo ndiyo zilikuwa zinafanyika kutoka kwa mkandarasi wetu. Ni moja ya majengo ambayo yapo kwenye hatua za ukamilishwaji na yatakapokuwa yamekamilika yatakabidhiwa ili askari wetu wasipate shida hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wengi mlikuwa bado mnafuatilia, nimeshazunguka mikoa yote kasoro mikoa minne na kwa Mheshimiwa Sikudhani nitafika, bado Ruvuma, Njombe, Songwe, Geita pamoja na Singida. Nimetambua ukubwa wa tatizo hili na sisi ndani ya Serikali tunaendelea kuwasiliana kuweza kuhakikisha kwamba tunalibeba kwa ukubwa wake na hivyo tutalifanyia kazi ili kuweza kupatikana jawabu la kudumu linalohusu makazi ya askari wetu ili waweze kuendana na hadhi ya kazi wanazozifanya.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba za makazi Askari Polisi na Magereza katika Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma? (b) Je, Serikali imejipangaje kufanya ukarabati kwa nyumba za askari zilizopo Wilayani Tunduru ambazo kwa muda mrefu hazijafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Ni miaka saba sasa nikiwa hapa Bungeni swali hili linapoulizwa majibu ni haya haya, hayajawahi kubadilika hata siku moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna changamoto kubwa zaidi kwa hao wenzetu polisi kwa sababu kuwalaza polisi uraiani wakati huohuo ukawatuma kwenda kufanya operesheni ambazo zitapelekea kuwapiga wananchi, ni hatari kwao na kwa familia zao. Ni lini Serikali itafanya mkakati wa makusudi kabisa kuhakikisha kwamba imeleta majibu tofauti na haya ili wananchi wa Rombo waone nyumba za polisi zinajengwa, waone nyumba za askari magereza zinajengwa, badala ya majibu haya ya kisiasa yanatolewa kila mwaka?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niliweke sawa swali la shemeji yangu Mheshimiwa Selasini. Suala la majibu kuwa yanafanana ni kwa sababu kila mwaka pia tunaajiri, kwa hiyo tutatarajia upungufu uendelee kuwepo, hiyo ni mathematically. Suala la jibu kuwa lilelile si kwamba Serikali haifanyi kitu, hivi tunavyoongea ukiangalia Dar es Salaam tu kuna nyumba zaidi ya 300 zinajengwa lakini hazitatosha kwa sababu mwaka jana pia tumeendelea kuajiri na kwa kuwa tunaendelea kuajiri maana yake mahitaji yale yataendelea kuongezeka kadri tunavyoajiri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu iliyopita mmeona imejenga majengo mengi tu tena ya ghorofa, ndiyo mengine kama haya ya Mara ambayo Mheshimiwa Vedastus ameyaongelea. Mwezi uliopita, Mheshimiwa Rais ametoa shilingi bilioni 10 kwa upande wa magereza na ujenzi unaendelea. Kwa maana hiyo ujenzi utaendelea lakini na mahitaji yataendelea kwa sababu tunaendelea kuajiri, hata mwaka huu tunategemea tuendelee kuajiri kwa sababu bado idadi ya askari ambao wanatakiwa haijatosheleza. Kwa maana hiyo tumelipa uzito unaostahili suala hili lakini hatuwezi kuacha kuongeza vijana kwa sababu hakuna nyumba, tutaendelea kuongeza vijana lakini tutaendelea kujenga nyumba ili vijana waweze kupata nyumba hizo.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba za makazi Askari Polisi na Magereza katika Wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma? (b) Je, Serikali imejipangaje kufanya ukarabati kwa nyumba za askari zilizopo Wilayani Tunduru ambazo kwa muda mrefu hazijafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 4

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Wilaya ya Kilolo imeanza toka mwaka 2002 takribani sasa ni miaka 15, lakini kwa muda mrefu OCD amekuwa akikaa tarafa nyingine na makao makuu yako Tarafa nyingine na inabidi kuwasafirisha mahabusu kwani wako kule anakokaa OCD zaidi ya kilomita 100 kuwapeleka katika tarafa nyingine ya Kilolo. Kama Serikali yenyewe bado haijajiweka vizuri, kwa nini isitumie National Housing au NSSF kujenga nyumba pale Kilolo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo tumekuwa tukieleza kila siku na leo vilevile, mipango ya ujenzi wa nyumba upo njiani. Kwa hiyo, hakuna haja ya kufikiria kwamba labda suala la OCD wa Kilolo kutokuwa na nyumba halijatiliwa maanani. Namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, pale ambapo mipangilio yetu itakapokamilika na mikataba itakapokuwa imesainiwa, basi ujenzi huo utaanza na tatizo ambalo linamkumba OCD wetu huyo wa Kilolo na Ma-OCD wengine popote nchini litakuwa limepata ufumbuzi.