Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 25 2017-04-10

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY (K.n.y MHE. ESTHER A. MAHAWE) aliuliza:-
Vituo vya Afya na Zahanati zilizo karibu na Hospitali za Wilaya zina changamoto ya utoaji huduma bora kwa sababu ya upungufu wa dawa na watumishi wa kada ya afya hivyo kusababisha kuhudumiwa na Hospitali za Wilaya ambazo bajeti za dawa hazikidhi:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza bajeti ya Hospitali za Wilaya zilizoko katika Mkoa wa Manyara?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rai, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Alexander Mahawe, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa wa Manyara kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa 2016/2017, Halmashauri za Mkoa wa Manyara zimetengewa bajeti ya shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya. Kati ya fedha hizo, fedha zilizopokelewa hadi Machi, 2017 ni shilingi bilioni 1.07 sawa na asilimia 75%. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Halmashauri za Mkoa huo zimepanga kutumia shilingi 1.58 kwa ajili ya dawa sawa
na ongezeko la asilimia 9.7 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017.
Mheshimiwa Spika, Serikali imedhamiria kuanza kutumia mfumo wa kupeleka fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa moja kwa moja katika vituo vya tiba yaani Direct Facility Financing (DFF), hali itakayosaidia vituo vya kutolea huduma kuboresha upatikanaji wa dawa kwenye hospitali,
vituo vya afya na zahanati. Halmashauri zitabaki na jukumu la kusimamia taratibu zote na kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.