Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY (K.n.y MHE. ESTHER A. MAHAWE) aliuliza:- Vituo vya Afya na Zahanati zilizo karibu na Hospitali za Wilaya zina changamoto ya utoaji huduma bora kwa sababu ya upungufu wa dawa na watumishi wa kada ya afya hivyo kusababisha kuhudumiwa na Hospitali za Wilaya ambazo bajeti za dawa hazikidhi:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza bajeti ya Hospitali za Wilaya zilizoko katika Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri niwashukuru Naibu Waziri wa Afya na Naibu Waziri wa TAMISEMI kwa kuja Mbulu na kutembelea baadhi ya Halmashauri za Wilaya ya Mbulu na vituo hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika swali la msingi muuliza swali alitaka pia mpango mkakati wa Serikali kuajiri kada za afya kwa maelezo ya swali la msingi. Je, Serikali ina mkakati gani na ajira ya kada za afya ili kupunguza tatizo
hili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ongezeko la asilimia 9.7 ni dogo sana ukilinganisha na tatizo la huduma ya afya hususan dawa na vifaa tiba katika nchi yetu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kukaa chini na kwenda katika Halmashauri zote nchini kufanya tafiti ili waweze kuleta mpango mkakati wa kuondoa tatizo la
upungufu wa dawa na vifaa tiba katika nchi yetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza mpango mkakati wa Serikali ni suala zima la ajira kama tulivyosema. Niseme wazi kwamba ajira zilisimama kwa lengo mahususi kutokana na mipango ya Serikali na hapa juzi mnaona kwamba mchakato wa ajira za elimu hasa walimu wa sayansi umeanza lakini sio muda mrefu kwa kadri Ofisi ya Rais, Utumishi itakavyokuwa imejipanga itatoa vibali vya ajira kwa ajili ya sekta ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba tuondoe hofu katika suala hilo kwa sababu tunajua wazi kwamba kweli tuna changamoto ya wahudumu mbalimbali hasa katika sekta ya afya katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la
mpango mkakati ni kweli, kwanza naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge leo hii ukifanya reference katika Halmashauri zetu kuna ma-DMO wengi sana walikuwepo hapa Mkoani Dodoma. Lengo ni kuhakikisha sasa tunatengeneza mipango mizuri na sio ile mipango ya mezani peke yake; tunatengeneza mipango mizuri ya kwenda kujibu matatizo ya afya katika maeneo yetu. Leo hii tumesema fedha zitakwenda moja kwa moja mpaka katika kituo cha afya
na zahanati; tumepata akaunti zote za vituo vya afya katika nchi yetu; huo ni mpango mkubwa kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba
niwaeleze ndugu zangu wakati mwingine tuna tatizo kubwa la usimamizi wa rasilimali fedha. Katika mwaka 2016/2017, mpaka mwezi Julai kuna outstanding fedha ambazo ni za Basket Fund hazijatumika karibu bilioni 20. Katika Mkoa wa Manyara peke yake kuna karibu milioni 500 mpaka mwezi Julai zilikuwa hazijatumika. Mpaka tunapozungumza leo hii bajeti yetu ya mwaka huu Basket Fund ni zaidi ya shilingi bilioni 106.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mpaka mwezi
Desemba fedha zile ambazo zimekuwa accrued ambazo hazijatumika na fedha zilizoingia ni takriban shilingi bilioni 71; kati ya fedha hizo 71, fedha ambazo zimetumika mpaka hivi sasa ni asilimia 55 tu mpaka mwezi Desemba, nini maana
yake? Fedha zipo katika Halmashauri yetu lakini dawa hakuna.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwasihi Waheshimiwa
Wabunge kwamba tuhakikishe katika Halmashauri zetu fedha za Basket Fund tuwabane ma-DMOs na wahasibu wetu tuweze kuzibainisha ziende zikanunue dawa na vifaa tiba; lengo kubwa ni kumwokoa mwananchi wa Tanzania.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY (K.n.y MHE. ESTHER A. MAHAWE) aliuliza:- Vituo vya Afya na Zahanati zilizo karibu na Hospitali za Wilaya zina changamoto ya utoaji huduma bora kwa sababu ya upungufu wa dawa na watumishi wa kada ya afya hivyo kusababisha kuhudumiwa na Hospitali za Wilaya ambazo bajeti za dawa hazikidhi:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza bajeti ya Hospitali za Wilaya zilizoko katika Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 2

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tatizo lililopo Manyara linafanana kabisa na tatizo lililopo Wilaya ya Kakonko. Tatizo ambalo lipo Hospitali ya Wilaya ya Kakonko ambayo ni kituo cha afya haijapata hadhi ya Wilaya ni kupata dawa zenye hadhi ya kituo cha
afya lakini zinatumiwa na wananchi wa Wilaya nzima kama Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri alitembelea Kakonko akaona hali ya kituo cha afya ilivyo…
MHE. KASUKU S. BILAGO: Ndiyo nauliza hivyo; ni lini sasa Kituo cha Afya Kakonko kitabakia kuwa kituo cha Afya ili iweze kujengwa Hospitali ya Wilaya ya Kakonko?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kweli nikiri kwamba, nimefika pale Kakonko na nimetembelea kile kituo cha afya tukiwa pamoja na Mbunge ni kweli kuna changamoto hizo kubwa lakini tubaini kwamba vipaumbele hivi mchakato wake unaanza kiwilaya. Hata hivyo, Mheshimiwa Bilago anafahamu kwamba pale alikuwa hana ambulance; Serikali imepeleka tayari ambulance kipindi hiki kifupi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika mpango wa bajeti katika Basket Fund yake ana milioni 395, fedha ambayo nimpe taarifa mpaka mwezi wa Saba Halmashauri yake zaidi ya shilingi 197 zilikuwa hazijatumika zimevuka mwaka wakati
wananchi wana matatizo. Kwa hiyo, naomba niseme sisi kama Serikali tutaangalia jinsi gani tutafanya katika mchakato huu ili kwenda pamoja na wenzetu wa Halmashauri, lakini jambo la msingi ni lazima tuwasimamie watendaji wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingine kuna
baadhi ya wengine wanafanya mambo ya hovyo na wananchi wanaendelea kupata shida wakati fedha zipo; Mbunge na watu wengine wanapata matatizo kumbe fedha zipo watendaji wetu wameshindwa kutimiza wajibu wao. Kwa hiyo, tupo pamoja kuhakikisha mambo yanaenda vizuri
katika Halmashauri zetu.