Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 20 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 168 2017-05-09

Name

Haji Khatib Kai

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:-
Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeimarisha kwa kuweka boti kwa ajili ya Police Marine maeneo mengi ya mito, maziwa na hata baharini ili kuzuia au kudhibiti ajali zinapotokea.
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma hiyo katika Mikoa au Wilaya ambazo hazijapata huduma hiyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Khatib Kai, Mbunge wa Micheweni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na mpango wa kupeleka huduma za boti kwa ajili ya Polisi Wanamaji ili kuzuia, kudhibiti ajali kwa awamu katika mikoa yote na Wilaya ambazo hazijapata huduma pale uwezo wa kibajeti utakapoimarika.
Aidha, muda huu ambapo Serikali inaendelea kutafuta fedha ili huduma hizo ziweze kupatikana, huduma hiyo ya Polisi Wanamaji itatolewa na vituo vya Wanamaji waliopo karibu kwa kufanya doria kwenye maeneo husika.