Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Khatib Kai

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:- Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeimarisha kwa kuweka boti kwa ajili ya Police Marine maeneo mengi ya mito, maziwa na hata baharini ili kuzuia au kudhibiti ajali zinapotokea. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma hiyo katika Mikoa au Wilaya ambazo hazijapata huduma hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI KHATIB KAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumejengeka dhana ya askari wa KMKM kule Zanzibar kujiona wao peke yao ndio wenye haki ya kufanya doria baharini, jambo ambalo hupelekea askari hawa ambao ni askari Marine ambao wamepata mafunzo maalum kujiona wametelekezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana na mimi kwamba sasa ni wakati muafaka wa askari wa Police Marine - Pemba kupata boti ili aweze kufanya doria ya haraka ambayo itaweza kuokoa usalama kwa Pemba lakini kwa Watanzania kwa jumla? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa Jimbo langu la Micheweni, raia wema na raia wenye kupenda amani idumu nchi hii wamewahi kushika boti za Kisomali zaidi ya mara mbili; na boti hizi zinapofanyiwa upekuzi zimegundulika na maganda ya risasi.
Je, kwa kuwa askari wa Marine Pemba wanasema kila mwezi hutolewa mafuta lita 500 kwa ajili ya doria baharini, utakubaliana na mimi sasa kwamba ni vema Police Marine - Pemba kuwa na boti ya doria ili kuweza kuimarisha ulinzi wa baharini, lakini pia kuweza kunusuru usalama wa nchi hii na raia?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge juu ya umuhimu wa Police Marine - Pemba Micheweni kuwa na boti yake. Ndiyo maana katika jibu langu la msingi nilizungumza kwamba azma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba Wilaya zote ambazo zinapaswa kuwa na boti, polisi wanapatiwa kadri hali ya kibajeti itakavyoruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hiyo ndiyo azma ya Serikali na pale ambapo bajeti itakapokuwa inaruhusu, tutafanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na askari wa KMKM, Jeshi la Polisi kutokana na kutokuwa na vifaa vya kutosha ikiwemo uchache wa boti zilizomo katika maeneo mballimbali nchini, hufanya kazi kwa ushirikiano na vyombo vingine vya usalama nchini ikiwemo Kikosi cha KMKM.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme Mheshimiwa Mbunge ana bahati kwamba katika Wilaya yake ajue kwamba Jeshi la Polisi limekosa boti kwa wakati huu, lakini zipo boti za KMKM ambazo zinasaidiana na Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa pamoja kusimamia ulinzi katika upande wa bahari.

Name

Dr. Ally Yusuf Suleiman

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mgogoni

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:- Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeimarisha kwa kuweka boti kwa ajili ya Police Marine maeneo mengi ya mito, maziwa na hata baharini ili kuzuia au kudhibiti ajali zinapotokea. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma hiyo katika Mikoa au Wilaya ambazo hazijapata huduma hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. SULEIMAN ALLY YUSSUF: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ajali za baharini zimekuwa nyingi sana siku hizi na kadhalika majanga ya baharini (disasters) naiuliza Serikali: Je, imejipangaje kwa kujenga vituo karibu na bahari na pia kutumia sayansi ya kileo, yaani kutumia kama drowns ili kuweza kubaini haraka sehemu zilizofikwa na mabalaa na kuweza kutoa huduma ya mwanzo haraka sana? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie pia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua umuhimu wa kuimarisha usalama katika maeneo ya bahari hasa pale ajali zinapotokea. Ndiyo maana kwa kulitambua hilo, Serikali imeamua kuunda kikosi kazi cha coast guard ambapo Jeshi la Polisi ni taasisi mojawapo ambayo imo katika kikasi hicho. Kwa pamoja na mambo mengine, kikosi hicho kinaangalia masuala yote yanayohusu uokoaji pale majanga yanapotokea ikiwemo upatikanaji wa vifaa vya kisasa kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amezungumza.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:- Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeimarisha kwa kuweka boti kwa ajili ya Police Marine maeneo mengi ya mito, maziwa na hata baharini ili kuzuia au kudhibiti ajali zinapotokea. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma hiyo katika Mikoa au Wilaya ambazo hazijapata huduma hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa Wilaya ya Mafia imezungukwa na bahari na hakuna Police Marine na kuna matishio ya Maharamia wa Kisomali. Je, ni lini sasa Serikali itafikiria uwezekano wa kuleta doria ya Police Marine katika Kisiwa cha Mafia? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mafia ni kati ya maeneo ambayo tumeyawekea kipaumbele katika kuimarisha usalama katika maeneo ya bahari. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunalitambua hilo; na pale ambapo hali ya bajeti itakaporuhusu, tutalifanyia kazi.(Makofi)