Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 32 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 259 2017-05-23

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:-
Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika.
Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sura ya Nne aya ya 4.2.7 ya Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017 - 2020/2021) unasisitiza pamoja na mambo mengine upanuzi wa wigo wa vivutio vya utalii na utalii utokanao na vivutio vya urithi wa utamaduni (The heritage tourism)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu kwa kuzihusisha Halmashauri husika inakamilisha orodha ya vivutio vyote vya utalii ikiwa ni pamoja na vivutio vya malikale nchini ili kuweka utaratibu wa kuvisajili, kuviboresha na hatimaye kuvitangaza na kuviuza kwa watalii wa ndani na wa nje. Zoezi hili linatengemea kukamilika mwaka wa 2017/2018. Vivutio vya mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya na Jiwe linalocheza la Nyaburebeka vilivyoko katika kisiwa cha Ukara katika Halmashauri ya Ukerewe ni miongoni mwa vivutio hivyo.