Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:- Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri. Pamoja na majibu hayo naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Jumapili tulikuwa na semina inayohusu mambo ya utalii, na kwenye jarida hili kulikuwa na taarifa ambazo zilikuwa na upungufu juu ya vivutio hivi. Sasa Je, Waziri yuko tayari kutembelea visiwa vya Ukerewe na kushuhudia vivutio hivi ili awe Balozi mzuri na mwenye taarifa zilizo sahihi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, suala la ukuzaji
na uendelezaji wa vivutio hivi mbali na kuvitangaza inategemea zaidi ubora wa miundombinu ya kuvifikia vivutio hivi; na kwa kuwa Halmashauri zetu hazina uwezo wa kutosha wa kuboresha miundombinu hii, sasa Serikali iko tayari kuboresha miundombinu ya kufikia vivutio hivi hasa Jiwe linalocheza la Nyaburebeka la Kisiwani Ukara? (Makofi)

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niko tayari kabisa kutembelea vivutio hivyo pamoja na Mbunge, Mheshimiwa Mkundi bila wasiwasi wowote na tutapanga safari hiyo mwezi Agosti mwaka huu.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba vivutio vyote vya utalii vinakuwa vizuri zaidi kama vinafikika na raia na watalii wanaotaka kuvitembelea. Wakati tutakapotembelea tutafanya tathmini ya vivutio hivyo na kuona ni namna gani juhudi hizi zitakamilika ili vivutio hivyo vifikike.

Name

Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:- Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Katika Jimbo la Hai kuna kivutio cha Bwawa moja ambalo lina maji ya moto linaitwa Chemka. Wageni wamekuwa wakienda kule, lakini wanafika kwa kutumia kama vile njia za panya, lakini Serikali kama Wizara bado hawajakitambua kivutio kile na barabara ya kwenda kule ni mbaya sana. Swali langu, je, Serikali mpo tayari kwenda kukitembelea kituo kile cha maji ya moto na kukifanya official ili Serikali nayo iweze kupata mapato? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi tu anazungumzia juu ya kivutio ambacho kiko kwenye Wilaya ya Hai...
Tuko tayari kwenda kukagua lakini nilitaka kuweka nyongeza...

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:- Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kilometa 180 tu kutoka hapa kuelekea Kondoa – Irangi kuna malikale nzuri, kuna michoro ya mapangoni na miundombinu ya barabara imeimarika. Sasa nataka kujua Wizara hii husika itatengeneza vipi yale mazingira ya kule ili kuimarisha utalii pamoja na mafunzo katika mapango ya michoro ya kale Kondoa – Irangi? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi vivutio vyote vya utalii ambavyo vinaangukia kwenye eneo la heritage tourism vyote tumefanya utaratibu wa kuviorodhesha halafu baadaye tunavisajili. Kuvisajili maana yake ni pamoja na kuangalia viwango vyake vya ubora na kuona kama kweli vinakidhi haja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuwa tumepokea taarifa hizo kutoka kwenye Wilaya mbalimbali, baadaye hatua inayofuata ni kuvitembelea na kuvihakiki.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:- Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Hata Wilaya ya Karagwe tuna vivutio vingi vya malikale likiwemo eneo ambalo Chief Rumanyika alikaa. Je, Wizara imeweka vivutio vya malikale hizi kwenye orodha ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kivutio kinachohusu makazi ya Chifu Rumanyika ni moja tu kati ya vivutio vinavyohusu Machifu wetu wote nchi nzima kila eneo na kila Wilaya. Kwa hiyo, mpango wa Serikali ni kama nilivyoeleza hapo awali kwamba ni kuviorodhesha, kuvisajili, kuvikagua na kuona ubora wake na hatimae kuviuza kwa kuangalia sifa zake.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:- Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika. Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la moja. Kwa sababu Mheshimiwa Waziri ameonesha utayari wa kutembelea vivutio mbalimbali na kimsingi hajakuwa na ziara hivi karibuni ya kutembelea Nyanda za Juu Kusini ili akajionee maporomoko ya pili Afrika ya Kalambo pamoja na Ngome ya Bismark iliyoko Kasanga. Je, katika mwezi huo Agosti aliojipanga atatembelea na Nyanda za Juu Kusini?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ukanda wa Kusini ni eneo ambalo sasa hivi kama Taifa tunaliangalia kuwa ni eneo la kupanua shughuli za utalii nchini kwa maana ya kufanya kwamba utalii sasa unakwenda kila eneo nchi nzima na si upande wa Kaskazini peke yake. Kwa hiyo, kwa ufupi jibu ni kwamba; kipindi hicho kitakapofika tutatembelea pia Ukanda wa Kusini ikiwa ni pamoja na maporomoko ya Kalambo.