Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 59 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 487 2017-07-04

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:-
Wilaya ya Serengeti ni kitovu cha utalii na ni Wilaya inayopata watalii wengi lakini haina Hospitali ya Wilaya na hivyo kuleta usumbufu kwa wageni pamoja na wakazi wa Serengeti:- Je, ni lini Hospitali ya Wilaya itakamilika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Halmashauri
ya Wilaya ya Serengeti haina hospitali ya Wilaya, hivyo wananchi hutumia Hospitali Teule ya Nyerere yaani DDH ambayo inamilikiwa na Kanisa la Mennonite Tanzania. Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti ulianza mwaka 2009 katika Kijiji cha Kibeyo ambao unafanyika kwa awamu. Katika awamu ya kwanza, jumla ya shilingi bilioni 5.4 zilikadiriwa kutumika kwa ajili ya kuandaa michoro, kuanza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje, pamoja na jengo la upasuaji (operating theater). Fedha hizo zinatarajiwa kupatikana kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo ruzuku kutoka Serikali Kuu, Mfuko wa Maendeleo wa Halmashauri, Benki ya Maendeleo ya Afrika, pamoja na mapato ya ndani ya Halmashauri (own source).
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa uandaaji wa michoro pamoja na jengo la upasuaji lenye vifaa vyote (operating theater) vimekamilika na kukabidhiwa kwa Halmashauri tayari kwa matumizi. Aidha, ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) upo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji. Mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imeweka mpango wa kupeleka fedha ili jengo la wagonjwa wa nje (OPD) liweze kukamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kukamilisha ujenzi wa hospitali mbalimbali za Wilaya hapa nchini ili kuwasaidia wananchi kupata huduma bora za afya.